• ZEAS
  • EMIS
  • E-OFFICE
  • AJESR
  • ZanVibali
MOEVT
  • Home
  • About Us
  • News and Events
  • Staff Mail
  • Contact Us
  1. Vous êtes ici :  
  2. Accueil
  3. News and Events

MOEVT NEWS&EVENTS

UTIAJI SAINI MoU YA KUENDESHA MAFUNZO YA GROUND HANDLING KIST.

Détails
11 septembre 2023
374

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar imesema, inaunga mkono mpango ulioandaliwa na Taasisi ya  Sayansi na Teknolojia ya Karume (KIST), katika utowaji wa mafunzo ya huduma za ndege katika Viwanja vya Ndege.

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Bw.Khamis Abdalla Said, amesema hayo alipokuwa katika hafla ya utiaji saini makubaliano ya utowaji wa mafunzo hayo kwa Taasisi ya Karume  na Wataalamu wa huduma za ndege katika viwanja vya ndege, hafla ilifanyika katika  Ukumbi wa Mkutano wa Dkt. Idrissa Muslim Hijja Bweni Zanzibar.


Amesema, hatua hiyo inakwenda sambamba na dhamira ya Serikali juu ya kuimarisha usafiri wa anga hapa nchini.

Amesema, kuwepo kwa mafunzo hayo itachochea kupatikana Wafanyakazi wa kutosha wenye utaalamu wa kutoa huduma kwa kiwango kinachohitajika.

Aidha, Bw.Said amefahamisha kuwa, Vijana wengi wanamaliza elimu zao na kubakia mitaani kufanya mambo yasiostahiki hivyo, kuwepo kwa mafunzo hayo itakuwa chachu ya kutimiza ndoto zao na kuipunguzia mzigo Serikali.

Lire la suite...

MAFUNZO YA URATIBU WA WAZI WA KUPIMA UTENDAJI KAZI WA WATUMISHI

Détails
11 septembre 2023
357

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar bwana Khamis Abdulla Said amesema ili kufikia  malengo ya sekta ya Elimu ipo haja ya kuendelea kuwajengewa uwezo watendaji mbalimbali kwanzia viongozi hadi wanaowasimamia.

 

Amesema hayo wakati wa kufungua Mafunzo ya Uratibu wa wazi wa kupima utendaji kazi wa watumishi katika  ukumbi wa mikutano wa chuo cha Utalii Maruhubi Mkoa wa Mjini Magharib Unguja.


Amesema kuwepo kwa Mafunzo husaidia kufikia malengo ya taasisi husika kwa wakati. Amewataka washiriki hayo kuitumia  vyema fursa hiyo na kuyafata kwa  vitendo ili kufikia malengo ya taasisi zao.

Lire la suite...

HAFLA YA UGAWAJI WA VIFAA KWA WANAFUNZI KATIKA SKULI YA KENGEJA, PEMBA

Détails
11 septembre 2023
268

Mkurugenzi Idara ya Elimu Mbadala na Watu Wazima Bi Mashavu Abdallah Fakihi amesema Idara itaendelea kufanya jitihada za kuwarejesha katika mfumo rasmi wa Elimu waliotoroka na Waliokosa huduma hiyo.

Bi Mashavu ameyasema hayo wakati Akizungumza na Wazazi pamoja na Wanafunzi wa Elimu Mbadala kwa nyakati tofauti katika Hafla ya Ugawaji wa Vifaa kwa Wanafunzi huko katika Skuli ya Kengeja Wilaya ya Mkoani  na Skuli ya Uwandani Wilaya ya Chake Chake ikiwa nishamrashamta za kuelekea kilele Cha Maadhimisho ya Wiki ya Elimu ya Watu Wazima.

Amesema Idara imeshapiga hatua kwa asilimia 90 kupitia Mradi unaofadhiliwa kwa Mashirikiano ya pamoja kati ya UNICEF, Qatar na SMZ wenye Lengo la kuwarejesha Wanafunzi waliotoroka Skuli.

Aidha Bi Mashavu amesema  ugawaji wa vifaa utawasaidia Wanafunzi hao kuweza kupata hamasa na hamu yakuendelea na masomo na kujikomboa katika maisha yao ya baadae.

Lire la suite...

UFUNGAJI WA WIKI YA MAONESHO YA ELIMU YA JUU HUKO KATIKA UWANJA WA GOMBANI, PEMBA.

Détails
5 septembre 2023
413

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Nd. Khamis Abdullah Said amesema Kufanyika kwa Maonesho ya Wiki ya Elimu ya Juu Kisiwani Pemba Kuna lengo la kuwasogezea Wanafunzi huduma kwa ukaribu ili waweze kufanya maamuzi sahihi ya Kimasomo.

Ameyasema hayo wakati akifunga Wiki ya Maonesho ya Elimu ya Juu huko katika Uwanja wa Gombani Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba.

Amewataka Wanafunzi  pamoja na Wazazi kuyafanyia kazi maelekezo waliyoyapata kutoka  Vyuo mbali mbali  kabla ya kutoa maamuzi yao.

Akizungumzia jitihada za Serikali katika kuwapatia Wanafunzi fursa za kujiendeleza kielimu Katibu Mkuu amesema Serikali inafanya utaratibu wa kubadilisha sheria ya Bodi ya Mikopo Zanzibar ili huduma zao ziweze kupatikana hadi ngazi ya Stashahada.

Akifafanua zaidi Nd. Said amesema  Serekali zote mbili ya Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania na Serekali ya Mapinduzi Zanzibar kwasasa zinatoa huduma ya mikopo ili kujiendeleza kuanzia Ngazi ya Shahada.

Lire la suite...

KUFUNGA KIKAO CHA TATHMINI YA NUSU MWAKA YA MRADI WA KUIMARISHA UBORA WA ELIMU YA SEKONDARI ZANZIBAR

Détails
5 septembre 2023
395

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Zanzibar bwana Khamis Abdulla Said amesema, ni muda sasa kwa kila mwalimu kuchukua hatua ili kuhakikisha Zanzibar inaendelea kupata matokeo mazuri zaidi.

Amesema hayo wakati wa kufunga kikao cha tathmini ya nusu mwaka ya Mradi wa kuimarisha ubora wa Elimu ya Sekondari Zanzibar, Katika ukumbi wa mikutano Golden Tulip uwanja wa ndege Mjini Unguja.

Amesema, ili Walimu waendelee kufanya kazi kwa juhudi kubwa Wizara itaendelea kufanya kila namna kwa kushirikiana na wadau mbalimbali  kuhakikisha Walimu nao wanaendelea  kupewa Mafunzo ili kuendana na  mabadiliko ya Teknolojia. 

Amesema, Zanzibar ili iendelee kupata matokeo mazuri ipo haja ya kila muhisika  kutimiza wajibu wake kwa kuengeza bidii zaidi.

Lire la suite...

Page 10 sur 19

  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14

Contact Details

P.O.Box 394 Mazizini, Zanzibar
+255 24 223 2827
info@moez.go.tz

Main Menu

  • Home
  • About Us
  • News and Events
  • Staff Mail
  • Contact Us

Get in Touch

P.O.Box 394 Mazizini, Zanzibar
info@moez.go.tz

Our Institute

  • Kwarara Media Education Centre (KMEC)
  • The State University of Zanzibar (SUZA)
  • Vocational Training Authority(VTA)
  • Zanzibar Higher Education Loan Board(ZHELB)
  • Karume Institute of Science and Technology(KIST)
  • Zanzibar Examination Council(ZEC)
  • Zanzibar Institute of Education(ZIE)

External Links

  • Ministry of Education, Science and Technology (MOE)
  • The National Examination Council of Tanzania (NECTA)
  • The National Council for Technical Education (NACTE)
  • Tanzania Commission for University (TCU)
© MoEVT. Designed by ICT-Department.