
Serikali inaendelea kuimarisha miundombinu na kitekeleza Miradi ya kimkakati ili kuiwezesha Zanzibar kutumia rasilimali zake ili kufikia malengo ya uchumi wa bluu.
Ameyasema hayo wakati akifungua Mafunzo Maluum ya kuwajengea uwezo maafisa viungo wa Mradi wa Sebep katika suala zima la ujumuishaji wa kijinsia katika ukumbi wa Mikutano Chuo Kikuu cha Taifa (SUZA) Kampasi ya Maruhubi Mkoa wa Mjini Maharibi
Amesema mradi huo utasaidia Taifa kufikia malengo yake kutokana na mazingira ya nchi. Pia amesema mafanikio ya mradi huo yatafikiwa kwa wakati na ufanisi iwapo utazingatia masuala ya jinsia.