- Details
- 585
Utekelezaji wa Mikutano ya Tathmini ya Elimu ya Zanzibar ni kilelezo tosha cha Serikali inayozingatia misingi ya utawala bora katika kuwaongoza na kuwaletea maendeleo wananchi wake katika nyanja mbali mbali ikiwemo Sekta ya Elimu.
Utekelezaji wa Mikutano ya Tathmini ya Elimu ya Zanzibar ni kilelezo tosha cha Serikali inayozingatia misingi ya utawala bora katika kuwaongoza na kuwaletea maendeleo wananchi wake katika nyanja mbali mbali ikiwemo Sekta ya Elimu.
Uongozi wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar pamoja na wafanyakazi wote Leo tarehe 7/03/2024, wamesoma hitma ya kumuombea dua Aliye kuwa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo kuanzia Mwaka 1964 hadi 1965 ambae pia ni Rais Mstaafu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Alhaj Mzee Ali Hassan Mwinyi. iliyo fanyika katika Mskiti wa Jamii _Zej-Bar huko mazizini - Unguja.
Mhe.Lela Muhamed Mussa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar amesema , Wizara itaendelea kushirikiana na Wadau mbali mbali wa Elimu ili kuleta maendeleo bora katika sekta hiyo.
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe. Lela Muhamed Mussa ameipongeza Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Arusha kwa muundo mzuri wa utoaji wa elimu ambao unazalisha wataalamu wenye weledi unaowezesha wahitimu kuweza kujiajiri mara baada ya kuhitimu.
Mhe. Lela amesema hayo machi 5, 2024 alipotembelea Taasisi hiyo kwa lengo la kujifunza na kujionea shughuli mbalimbali zinazotekelezwa ikiwa ni kuona namna ya taasisi na vyuo vya elimu ya juu nchini Tanzania vinavyojiendesha.
“Nampongeza Uongozi wa Taasisi kwa uwekezaji mkubwa mlioufanya na kitu kikubwa nilichojifunza katika taasisi hii ni kujikita katika kufanya tafiti na sisi tumekuja kujifunza ili kuleta magaeuzi kupitia chuo Kikuu cha Zanzibar (SUZA) ili kuangazia taasisi zetu ambazo tunaweza kuzikita katika masuala ya tafiti ili kutatua changamoto mbalimbali za jamii” amesema Mhe.Lela
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe. Lela Muhamed Mussa, amefanya ziara ya ndani katika Ofisi za Baraza la Mitihani la Zanzibar, huko Vuga Wilaya ya Mjini Mkoa wa Mjini Magharibi.