Mhe.Lela Muhamed Mussa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar amesema , Wizara itaendelea kushirikiana na Wadau mbali mbali wa Elimu ili kuleta maendeleo bora katika sekta hiyo.
Mhe.Lela Muhamed Mussa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar amesema , Wizara itaendelea kushirikiana na Wadau mbali mbali wa Elimu ili kuleta maendeleo bora katika sekta hiyo.
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe. Lela Muhamed Mussa ameipongeza Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Arusha kwa muundo mzuri wa utoaji wa elimu ambao unazalisha wataalamu wenye weledi unaowezesha wahitimu kuweza kujiajiri mara baada ya kuhitimu.
Mhe. Lela amesema hayo machi 5, 2024 alipotembelea Taasisi hiyo kwa lengo la kujifunza na kujionea shughuli mbalimbali zinazotekelezwa ikiwa ni kuona namna ya taasisi na vyuo vya elimu ya juu nchini Tanzania vinavyojiendesha.
“Nampongeza Uongozi wa Taasisi kwa uwekezaji mkubwa mlioufanya na kitu kikubwa nilichojifunza katika taasisi hii ni kujikita katika kufanya tafiti na sisi tumekuja kujifunza ili kuleta magaeuzi kupitia chuo Kikuu cha Zanzibar (SUZA) ili kuangazia taasisi zetu ambazo tunaweza kuzikita katika masuala ya tafiti ili kutatua changamoto mbalimbali za jamii” amesema Mhe.Lela
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe. Lela Muhamed Mussa, amefanya ziara ya ndani katika Ofisi za Baraza la Mitihani la Zanzibar, huko Vuga Wilaya ya Mjini Mkoa wa Mjini Magharibi.
Balozi wa Canada nchini Tanzania Mhe.Kyle Nunas amesema Canada itaendelea kushirikiana na kuisaidia Tanzania hasa katika sekta ya elimu.
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe. Lela Muhamed Mussa ameshiriki katika hafla ya utiaji saini
Makubaliano (MoU) baina ya Karume Institute Of Technology (KIST) na Vocational Education and Training Authority (VETA) katika Ukumbi wa Mkutano wa KIST Mbweni - Mkoa wa Mjini Magharib.