![](/images/WhatsApp%20Image%202023-09-26%20at%209.46.17%20PM.jpg)
- Details
- 1284
Kufanya kazi kwa bidii katika utowaji wa Taaluma kutasaidi kuleta Mabadiliko na Maendeleo yaliyo bora kwa Taifa.
Amesema hayo katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Bw. Khamis Abdulla Said, wakati akifunga mafunzo ya Siku mbili yaliyo andaliwa kwa mashirikiano ya Idara ya Elimu Mbadala na Tume ya Taifa UNESCO kutoka Jamuhuri ya Muungano Tanzania. iliyofanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Elimu Mbadala Rahaleo Mjini Unguja.
Amesema, kuna baadhi ya Wakufunzi hawawajibiki ipasavyo jambo ambalo hupelekea kurudisha nyuma maendeleo ya elimu nchini.
Aidha, amewataka Wakufunzi hao waliopatiwa mafunzo kuyatumia ipasavyo kwa kuwapa vijana ujuzi uliobora utakao weza kuwasaidia katika Maisha yao ya Baadae.
Aidha, Bw. said amelishukuru shirika la Taifa (UNESCO) kwa kuandaa Mradi huo na kuuwasilisha kwa lengo la kutaka kuwaengezea ujuzi Wakufunzi wa Idara ya Elimu Mbadala.