• EMIS
  • E-OFFICE
  • Home
  • About Us
  • News and Events
  • Staff Mail
  • Contact Us
  1. You are here:  
  2. Home
  3. News and Events

MOEVT NEWS&EVENTS

WALIMU WA JUMUIYA YA WALIMU WANAWAKE WA MANISPAA YA MOROGORO WATEMBELEA ZANZIBAR

Details
22 September 2023
67

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar imesema, Itaendelea kuimarisha ushirikiano uliopo kati  ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali  Zanzibar na Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia,   ili kuwapatia elimu bora na yenye kukidhi mahitaji  wanafunzi wa pande zote mbili.

Naibu Waziri wa Wizara hiyo Mhe. Ali Abdul gulam Hussein, ameeleza hayo alipokuwa akizungumza na Walimu wa Jumuiya ya Walimu Wanawake wa  Manispaa ya Morogoro waliofika zanzibar kwa ziara maalum huko katika Ukumbi wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mazizini Unguja.

Amesema, Malengo ya Waasisi wa Nchi ya Tanzania ni kujenga umoja ambao utaleta maendeleo katika nyanja mbali mbali za kiuchumi ambayo chimbuko lake ni elimu.

Aidha Mhe. Gulam amewakumbusha walimu hao kutembelea zaidi maeneo ya kihistoria kwa ajili ya kuitangaza vyema zanzibar ili wanafunzi wa huko nao wawe na hamu ya kutembelea zanzibar kutokana na utamaduni na vivutio vyake.

Read more …

MASHIRIKIANO MAZURI NA WADAU MBALI MBALI KATIKA SEKTA YA LEO NI NJIA MOJA YA KULETA MAGEUZI YA ELIMU ZANZIBAR

Details
21 September 2023
89

Amesema hayo Meneja Rasilimali watu Tawala na Mipango Bi. Khadija Masoud Haji ambae pia  kaimu Mkurugenzi wa bodi ya Huduma za Maktaba,  akizungumza na Balozi wa Marekeni nchini Tanzania huko ofisini kwake  Mjini Unguja.

Amesema, Ili kuweza kusonga mbele katika Sekta ya Elimu basi ipo haja ya kuwa na mashirikiano mazuri na wadau mbali mbali wa Elimu.

Amesema, Bodi ya huduma za Maktaba Zanzibar, bado inahitaji mashirikiano ya kutosha ikiwemo upatikanaji wa Vifaa ili kuweza kutoa huduma bora kwa jamii.

Read more …

UZINDUZI WA TAMASHA LA 59 ELIMU BILA YA MALIPO MWAKA 2023 KISIWANI PEMBA

Details
20 September 2023
135

Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Salama Mbarouk Khatib, amezindua rasmi tamasha la elimu bila ya malipo, na kuwataka wanamichezo kufanya michezo kwa amani, utulivu na mshikamano.


Amesema kuwekwa kwa Wanafunzi kutoka Mikoa yote mitano ya Zanzibar, kukaa sehemu moja kunapelekea kujuana, kuendeleza amani na mshikamano baina yao.


Mhe.Salama  ameeleza hayo katika viwanja vya michezo Chuo cha mafunzo ya amali Vitongoji Wilaya ya Chake Chake, wakati wa uzinduzi wa tamasha la 59 elimu bila ya malipo mwaka 2023 Kisiwani Pemba.


“Sisi viongozi wenu munaotuona hapa tupo kitu kimoja, sasa na nyinyi wanafunzi kuwepo kwenu hapa kutoka maeneo tafauti ni kuendeleza umoja, amani na mshikamano ndani yake,”amesema.


Aidha mkuu huyo amesema michezo ni afya, hujenga umoja na heshima, hivyo kushiriki michezo kwa wanafunzi isiwe sababu ya kwenda kinyume na maadili ya kizanzibari.

Read more …

MKURUGENZI IDARA YA ELIMU SEKONDARI AKUTANA NA WALIMU WAKUU WA SKULI ZENYE WANAFUNZI WENGI WA KIDATO CHA NNE

Details
14 September 2023
169

Serikali kupitia wizara ya elimu inafanya kila jitihada ili kuhakikisha inaondosha kabisa alama ya zero kwenye  matokeo ya kidato cha nne.

Amesema hayo Mkurugenzi Idara ya Elimu Sekondari Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar bi Asya Iddi Issa wakati wa mkutano na Walimu Wakuu wa Skuli zenye Wanafunzi wengi wa kidato cha nne katika ukumbi wa Mikutano wa Mazizini Unguja. 


Akizitaja skuli ambazo  zinaongoza kuwa na wanafunzi wengi amesema ni skuli ya  Mwanakwerekwe C 410, Mtopepo  416, Kinuni 400 , na Nyerere 483.


Amesema idara yake ipo sambamba na Walimu hao ili kuendelea na mikakati ya kuhakikisha  Skuli hizo nazo zinaondoa kabisa alama ya zero.

Read more …

KATIBU MKUU AKUTANA NA WATENDAJI WAKE

Details
14 September 2023
142

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Bwana Khamis Abdulla Said  amesema Wizara ya Elimu ndio yenye dhamana ya kuhakikisha inaandaa vijana wa Taifa lao. Ameyasema hayo wakati alipokutana na watendaji wa Wizara hiyo huko Mazizini  Unguja.                 

Amesema Elimu ndio suala la Msingi katika Maendeleo ya kila Taifa,hivyo ni wajibu wa kila mtendaji kuhakikisha anafanya kazi kwa bidii na maarifa ili Taifa lizalishe wataalamu wazalendo.                        

Amesema Serikali itahakikisha kwamba kila mwananchi anapata fursa ya Elimu .

Akizungumzia  suala la miundombinu  ya Elimu,amesema atahakikisha kuwa kila mtu anahusika ili malengo hayo yafanikiwe.

Read more …

Page 1 of 12

  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10

Contact Details

P.O.Box 394 Mazizini, Zanzibar
+255 24 223 2827
info@moez.go.tz

Main Menu

  • Home
  • About Us
  • News and Events
  • Staff Mail
  • Contact Us

Get in Touch

P.O.Box 394 Mazizini, Zanzibar
info@moez.go.tz

Our Institute

  • Kwarara Media Education Centre (KMEC)
  • The State University of Zanzibar (SUZA)
  • Vocational Training Authority(VTA)
  • Zanzibar Higher Education Loan Board(ZHELB)
  • Karume Institute of Science and Technology(KIST)
  • Zanzibar Examination Council(ZEC)
  • Zanzibar Institute of Education(ZIE)

External Links

  • Ministry of Education, Science and Technology (MOE)
  • The National Examination Council of Tanzania (NECTA)
  • The National Council for Technical Education (NACTE)
  • Tanzania Commission for University (TCU)
© MoEVT. Designed by ICT-Department.