![](/images/WhatsApp%20Image%202023-09-13%20at%203.33.30%20PM%201.jpg)
- Details
- 462
Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Bwana Khamis Abdulla Said amesema Wizara ya Elimu ndio yenye dhamana ya kuhakikisha inaandaa vijana wa Taifa lao. Ameyasema hayo wakati alipokutana na watendaji wa Wizara hiyo huko Mazizini Unguja.
Amesema Elimu ndio suala la Msingi katika Maendeleo ya kila Taifa,hivyo ni wajibu wa kila mtendaji kuhakikisha anafanya kazi kwa bidii na maarifa ili Taifa lizalishe wataalamu wazalendo.
Amesema Serikali itahakikisha kwamba kila mwananchi anapata fursa ya Elimu .
Akizungumzia suala la miundombinu ya Elimu,amesema atahakikisha kuwa kila mtu anahusika ili malengo hayo yafanikiwe.