
Spika wa Baraza la Wawakilishi, Mhe. Zubeir Ali Maulid amesema, jitihada zinazochukuliwa na Serikali katika kujenga hamasa kwa Wanafunzi kusoma na kupata matokeo yaliyokuwa bora.
Ameyasema hayo alipokuwa akifungua Maonesho ya Juma la Elimu ya Juu kwa niaba ya Makamo wa Pili wa Rais huko Maisara, amesema, Maonesho hayo ni sehemu ya ubunifu wa Wizara ya Elimu katika kukuza huduma za kielimu.
Amesema, Serikali imekuwa inahitaji Wataalamu wa sekta mbali mbali ili kuendelea kufanya kazi nchini.
Amesema, hatua ya Wizara ya Elimu kuweka Maonesho hayo itafikiwa lengo ikiwemo Wanafunzi kujifunza kupitia Maonesho hayo ikiwemo kujua namna bora ya kujiunga na Vyuo mbalimbali vilivyopo nchini.