• ZEAS
  • EMIS
  • E-OFFICE
  • AJESR
  • ZanVibali
MOEVT
  • Home
  • About Us
  • News and Events
  • Staff Mail
  • Contact Us
  1. You are here:  
  2. Home
  3. News and Events

MOEVT NEWS&EVENTS

UFUNGAJI MAONESHO YA NNE YA WIKI YA WIKI YA ELIMU

Details
07 August 2023
418

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe. Lela Muhamed Mussa amesema, Serikali imedhamiria kuweka mazingira bora ya elimu kwa ngazi zote  ili kuleta maendeleo ya Kielimu nchini.

Ameyasema hayo wakati akifunga Maonyesho ya Nne ya wiki ya Elimu ya Juu, yaliyo fanyika katika Viwanja vya Maisara Mjini Unguja.

Ameseama, Maonyesho hayo   ni fursa kwa wazazi na wanafunzi katika kuendelea na elimu ya Vyuo Vikuu.

Amesema, wanafunzi  ni vyema kutumia fursa hiyo adhimu ya kupata kujiunga na Vyuo Vikuu kwa kwa urahisi ili kuweza kusonga mbele kielimu.

Mapema Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bw. Khamis Abdulla Said amesema, Idadi ya Wanafunzi  walofaidika  kujiunga na Vyuo Vikuu kupitia Maonesho hayo ni kubwa, jambo ambalo limesaidia sana kupunguza gharama za kutafuta tarifa za Vyuo husika.

Read more …

Maadhimisho ya Uhamasishaji wa Unywaji wa Maziwa kwa Wananchi na Watoto Maskulini na Majumbani.

Details
07 August 2023
320

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe. Lela Muhamed Mussa Amesema, kuwepo kwa Wafugaji wa Ng'ombe wa maziwa nchini ni msingi mzuri wa kuweza kuimarisha afya kwa jamii.

Ameyasema hayo wakati wa maadhimisho ya uhamasishaji wa unywaji wa maziwa kwa wananchi na watoto maskulini na majumbani, iliyo fanyika katika Viwanja vya Nane nane Dole Wilaya ya Magharib "A"Unguja.

Amesema, upo umuhimu mkubwa wa kunywa maziwa kwa binadamu hasa Watoto kwani watajengeka kiakili na kupelekea kufanya vizuri katika Masomo yao.

Aidha, amewaomba wazazi na walezi kuwapatia watoto maziwa angalau Lita Moja kwa Wiki kwani kufanya hivyo kutapunguza Madhara yanayotokana na  upungufu wa unywaji wa maziwa ikiwemo udumafu(Mulnutrition) pamoja na upungufu wa Damu mwilini.

Read more …

Mkutano wa 8 wa Wahandisi Wanawake, 2023.

Details
07 August 2023
406

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe. Lela Muhamed Mussa amesema, kuwepo kwa Wahandisi Wakike katika nchi kunapelekea kwenda sambamba na Mabadiliko ya Sayansi na Teknolojia nchini.

Ameyasema hayo wakati wa Ufungaji wa Mkutano wa 8 wa Wahandisi Wanawake, 2023- Uliondaliwa na Taasisi ya Wahandisi, Tanzania Kitengo cha Wanawake, uliyo fanyika katika Ukumbi wa Golden Tulip Bweni Unguja.

Aidha, amewaomba Wahandisi Wakike kutumia Fursa zinazotolewa na na Serikali.  ikiwemo kusajili Makampuni na kujiajiri kupitia Ukandarasi, kwani kufanya hivyo kutasaidia Maendeleo ya nchi kwa Ujumla.

Aidha, ameyapongeza Makundi mbali mbali ya Wahandisi Wanawake kwa Utendaji wao Mzuri, wakiwemo best CEO, best Researcher, best Engineer leader, best Company na best  Project. Kwa kupata zawadi inayojulikana kama "Mama Mhandisi Awards".

Read more …

Maonesho Yatasaidia Jamii Kuweza Kutambua Chuo na Usahihi wake,na Fani Zinazotolewa.

Details
04 August 2023
274

Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi Mhe Suleiman Massoud Makame ameipongeza Wizara ya Elimu Zanzibar kwa kuanzisha maonesho ya Wiki  ya Elimu ya Juu.

Amesema hayo wakati alipotembelea mabanda mbalimbali Katika maonesho ya 4 ya wiki ya Elimu ya Juu Maisara Unguja. 

Amesema maonesho hayo yatasaidia jamii kuweza kutambua chuo na usahihi wake,na fani zinazotolewa.

 Aidha amewataka Wanafunzi kujitokeza kwa wingi  Katika maonesho hayo ili kujua fursa mbalimbali zinazopewa kipaombele katika soko la ajira duniani.

Maonesho ni Njia Moja wapo ya Kurahisha na Kusaidia Wanafunzi Kuweza Kupata Huduma za Kitaaluma.

Details
04 August 2023
300

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Uchumi na Uwekezaji Mhe Mudrik Ramadhani Soraga amesema maonesho ni njia moja wapo ya  kurahisha na  kusaidia  Wanafunzi kuweza kupata huduma za kitaaluma ili waweze kukamisha ndoto za safar zao za Elimu .


Hayo ameyasema wakati akifanya ziara katika mabanda mbalimbali huko Maisara Mjini Unguja wakati wa maonesho ya 4 ya wiki ya Elimu ya juu Zanzibar.


Amesema maonesho hayo ni Chachu ya kutengeza daraja la juhudi za Serikali ya awamu ya nane Katika sekta ya Elimu nchini.

Ikiwa ni siku ya tatu ya maonesho ya 4 ya wiki ya Elimu ya Juu  vyuo,ambapo  Taasisi mbalimbali za kitaaluma na wajasiriamali  wameshiriki maonesho hayo huko Maisara Mkoa wa Mjini Magharib Unguja.

Page 13 of 18

  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17

Contact Details

P.O.Box 394 Mazizini, Zanzibar
+255 24 223 2827
info@moez.go.tz

Main Menu

  • Home
  • About Us
  • News and Events
  • Staff Mail
  • Contact Us

Get in Touch

P.O.Box 394 Mazizini, Zanzibar
info@moez.go.tz

Our Institute

  • Kwarara Media Education Centre (KMEC)
  • The State University of Zanzibar (SUZA)
  • Vocational Training Authority(VTA)
  • Zanzibar Higher Education Loan Board(ZHELB)
  • Karume Institute of Science and Technology(KIST)
  • Zanzibar Examination Council(ZEC)
  • Zanzibar Institute of Education(ZIE)

External Links

  • Ministry of Education, Science and Technology (MOE)
  • The National Examination Council of Tanzania (NECTA)
  • The National Council for Technical Education (NACTE)
  • Tanzania Commission for University (TCU)
© MoEVT. Designed by ICT-Department.