• ZEAS
  • EMIS
  • E-OFFICE
  • AJESR
  • ZanVibali
MOEVT
  • Home
  • About Us
  • News and Events
  • Staff Mail
  • Contact Us
  1. Está aquí:  
  2. Inicio
  3. News and Events

MOEVT NEWS&EVENTS

Hafla ya Kuwapongeza Walimu wa Kidato cha Sita kwa Upande wa Unguja kwa Matokeo Mazuri ya Mwaka 2022/2023

Detalles
14 Agosto 2023
363

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe. Lela Muhamed Mussa amesema, Kuoengezeka kwa kiwango cha ufaulu Zanzibar kutapelekea Kupiga hatua nzuri ya Kimaendeleo nchini.

Ameyasema hayo wakati wa hafla ya kuwapongeza Walimu wa Kidato cha Sita kwa upande wa Unguja kwa Matokeo mazuri ya mwaka 2022/2023. Hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa Skuli ya Sekondari Lumumba Mjini Unguja.

Amesema, ufaulu wa Kidato cha Sita umeongozeka kwa kiasi kikubwa jambo ambalo litapelekea kupatikana kwa Wataalamu bora nchini.

Aidha amesema, Walimu bado wanakazi kubwa ya kuleta Mageuzi katika Sekta ya  Elimu yenye kumlenga Mtoto katika kupata Elimu Bora itakayomsaidia katika maisha yake ya baadae.

Amesema, Wizara inatambua uwepo  changamoto ya Maabara kwa wanafunzi wa Sayansi. Hata hivyo Serikali inajitahidi kujenga Maabara za kisasa kuanzia ngazi ya Msingi hadi Sekondari ili kuleta ufaulu mzuri wa wanafunzi katika masomo hayo.

Lee más…

Hafla ya Kuzindua Kitabu cha Tathmini ya Gharama za Huduma ya Maji, Ujenzi wa Vyoo na Elimu ya Afya ya Mazingira katika Skuli.

Detalles
11 Agosto 2023
464

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Mh Leila Muhamed Mussa amesema wanathamini mchango mkubwa unaotolewa na Shirika la Maendeleo la UNISEF katika kutatua suala la maji katika Skuli za Zanzibar. 

Akizindua kitabu cha tathmini ya gharama za huduma ya Maji, ujenzi wa Vyoo na elimu ya afya ya mazingira katika Skuli hafla iliofanyika  katika ukumbi wa Madinatul Bahari Mbweni amesema mpango huo utaleta matukio mazuri kwa wanafunzi katika kujifunzia. 

Amesema  hatua hiyo  italeta matumaini ya kuondosha ongezeko la maradhi mbali mbali pamoja na wanafunzi kupelekea kuwa na mazingira wezeshi ya kuweza kujifunza na kuongeza ufaulu kwa wanafunzi hao. 

Hata hivyo Mh Leila amewaonba  wadau mbali mbali kuendele kuisaidia Zanzibar katika kutatua suala la vyoo na maji kwani licha ya jitihada zinazochukuliwa bado lipo katika Skuli zinazo wazunguka 

Lee más…

Hafla ya Uzinduzi wa Fani Mbili Mpya, Chuo Cha Taifa SUZA

Detalles
10 Agosto 2023
465

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar bwana Khamis Abdulla Said amesema kubuni fani mpya zitasaidia kuzalisha  wataalam wanaohitajika katika soko la ajira.


Amesema hayo katika  hafla ya uzinduzi wa  fani mbili mpya fani ya Shahada ya Sayansi ya Maabara Tabibu (bachelor of science in medical laboratory science) na fani ya 
shahada ya uzamili ya usimamizi wa biashara na fedha(Master of business administration in finance) katika ukumbi wa mikutano wa Chuo Cha Taifà SUZA huko Tunguu Mkoa wa Kusini Unguja.

Amesema fani hizo zitasaidia kupata wafanyakazi watakaosaidia kutatua changamoto ya vifaa vya afya  na kuleta mageuzi ya kiuchumi nchini.


Aidha akizunguzia suala la kufanya tafiti amesema tafiti zitasaidia Sana   Serikali  kufikia malengo ya kukuza uchumi kwa kujua changamoto na utatuzi wake kutokana na tafiti mbalimbali zitakazofanywa.

Lee más…

 Warsha Maalumu ya Labondogo Ilioratibiwa na Taasisi ya Afisi ya Raisi  Ufuatiliaji na Usimamizi wa Utendaji Serikalini

Detalles
10 Agosto 2023
452

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar bwana Khamis Abdulla Said amesema Wizara itahakikisha inafatilia na kufanyia kazi vipaombele vya sekta hiyo ili kufikia malengo ya kuendelea kuboresha sekta hiyo.


Amesema hayo wakati amefungua  warsha maalumu ya Labondogo   ulioratibiwa na kitengo maalumu cha Taasisi ya Afisi ya Raisi  Ufuatiliaji na Usimamizi wa utendaji Serikalini katika ukumbi wa mikutano Chuo Cha Utalii Maruhubi Mkoa wa Mjini Magharib Unguja.


Amesema atahakikisha Wizara ya Elimu inatekeleza vipaombele vya Raisi kwa kujenga  miundombinu imara, kuwajengea uwezo Walimu na Watendaji ili kukukuza ujuzi wao na kuweza kuzitumia vyema teknolojia na upatikanaji wa vifaa vya kufundishia na kujifunzia.


Amesema Katika kuandaa mkakati utakaohakikiksha utekeleza wa vipaombele hivyo vinafikiwa ili kupelekea kuzalisha wataalam wazalendo.

Lee más…

Mafunzo ya Siku Moja Dhidi ya Udhalilishaji Yaliyowashirikisha Wanafunzi wa Skuli ya Uondwe

Detalles
10 Agosto 2023
343

Mwanasheria Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Nd. Masudi Mohammed Haji amesema vitendo vya  udhalikishaji vinachangia kwa kiasi kikubwa kurejesha nyuma Maendeleo ya Kimasomo kwa Wanafunzi.

Amesema hayo wakati akifungua Mafunzo ya siku moja dhidi ya udhalilishaji yaliyowashirikisha Wanafunzi wa Skuli ya Uondwe huko katika ukumbi wa Skuli ya Uondwe Wilaya ya Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba 

Amesema kutokana na Vitendo hivyo Wanafunzi huathirika kisaikolojia na kupelekea changamoto kubwa kwa maendeleo yao.

Lee más…

Página 12 de 18

  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16

Contact Details

P.O.Box 394 Mazizini, Zanzibar
+255 24 223 2827
info@moez.go.tz

Main Menu

  • Home
  • About Us
  • News and Events
  • Staff Mail
  • Contact Us

Get in Touch

P.O.Box 394 Mazizini, Zanzibar
info@moez.go.tz

Our Institute

  • Kwarara Media Education Centre (KMEC)
  • The State University of Zanzibar (SUZA)
  • Vocational Training Authority(VTA)
  • Zanzibar Higher Education Loan Board(ZHELB)
  • Karume Institute of Science and Technology(KIST)
  • Zanzibar Examination Council(ZEC)
  • Zanzibar Institute of Education(ZIE)

External Links

  • Ministry of Education, Science and Technology (MOE)
  • The National Examination Council of Tanzania (NECTA)
  • The National Council for Technical Education (NACTE)
  • Tanzania Commission for University (TCU)
© MoEVT. Designed by ICT-Department.