• ZEAS
  • EMIS
  • E-OFFICE
  • AJESR
  • ZanVibali
MOEVT
  • Home
  • About Us
  • News and Events
  • Staff Mail
  • Contact Us
  1. Está aquí:  
  2. Inicio
  3. News and Events

MOEVT NEWS&EVENTS

UFUNGUZI WA MAADHIMISHO YA WIKI YA ELIMU YA WATU WAZIMA NA SIKU YA KUJUA KUSOMA NA KUANDIKA DUNIANI

Detalles
05 Septiembre 2023
421

Utoaji wa Elimu kwa wanafunzi utapelekea kuengezeka kwa ufaulu mzuri unaoendana samabmba na mabadiliko ya Sayansi na Teknolojia.

Amesema hayo Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Bw. Khamis Abdulla Said. wakati wa hafla ya Ufunguzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Elimu ya Watu Wazima na Siku ya kujua kusoma na kuandika duniani. Iliyo fanyika katika Uwanja wa  Maktaba ya Dunga Wilaya ya kati Unguja.

Amesema, Elimu Bora ni chanzo kikubwa cha mabadiliko katika sekta ya Elimu, hivyo Walimu wajitahidi kusomesha kwa bidii ili kuleta mabadiliko katika sekta hiyo.

Aidha, ametowa wito kwa wazazi na walezi kuwasimamia watoto Katika suala zima la kusoma, kuandika na kuhesabu  ili waweze kuwa imara na kuleta mabadiliko katika masomo yao.

Amesema,  Wizara inafanya jitihada ya kuanzisha Maktaba kwa kila Wilaya ili kuweza kuondoa changamoto ya kufata Maktaba  masafa marefu na kupelekea kuzorotesha maendeleo ya kielimu nchini.

Lee más…

WARSHA KWA WAANDISHI WA HABARI JUU YA MATUMUZI SALAMA YA VIDONGE LISHE KWA WANAFUNZI WALIOBALEGHE

Detalles
05 Septiembre 2023
337

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Dkt Mwanakhamis Adam Ameir amesema,  vyombo vya habari vinanafasi kubwa ya  kushajihisha jamii juu ya matumuzi salama ya vidonge vya  virutubisho.


Amesema hayo wakati alipofungua warsha kwa waandishi wa habari juu ya matumuzi salama ya vidonge lishe kwa Wanafunzi Waliobaleghe   huko Kituo Cha Walimu Kiembe Samaki Mkoa wa Mjini Magharib Unguja.


Amesema, Waandishi wanayo nafasi kubwa kwenye jamii hivyo nao ni njia moja wapo ya kuhakikisha wanafikisha ujumbe husika katika jamii.

 

Aidha amesema, kuipa jamii Taaluma hiyo ni kuepusha dhana potofu iliopo kwenye jamii juu ya matumuzi ya virutubisho hivyo.

Lee más…

KIKAO CHA KUTATHMINI MAENDELEO YA KISOMO CHA WATU WAZIMA

Detalles
05 Septiembre 2023
334

Mratibu Idara ya Utumishi na Uendeshaji Mwalimu Harith Bakar Waziri amesema kisomo cha Watu Wazima ni njia muhimu ya Kuwakomboa na Kutokujua kusoma, kuandika na kuhesabu.

Ameyasema hayo katika kikao cha Kutathmini Maendeleo ya Kisomo cha Watu wazima kilichowashirikisha Wanakisomo kutoka Wilaya nne za Pemba ikiwa ni miongoni mwa shamrashamra za Maadhimisho ya Juma la Kisomo cha Wtu wazima Huko katika Ukumbi wa Wizaraya Elimu na Mafunzo ya Amali Chake Chake Pemba.

Mwalimu Harithi amesema wakati dunia ikiadhimisha Wiki ya Kisomo kuna haja kubwa ya kutathmini maendeleo yaliyofikiwa katika kuwakomboa watu kuondokana na tatizo la kutokujua kusoma, kuandika na kuhesabu.

Akifafanua zaidi Mratibu huyo amesema kufanyika kwa Tathmini hio kutasaidia kujua ufahamu wa Wanakisomo hao  na namna ya kuweza kuwasaidia.

Aidha amewataka waratibu wa Kisomo cha Watu wazima pamoja na Walimu wanaowafundisha kisomo hicho kutumia lugha nzuri pamoja na kuwapa mashirikiano Wanakisomo hao.

Nae Mratibu Idara ya Elimu Mbadala na Watu Wazima Nd. Salim Kuza Sheikhan amewataka wanakisomo cha Watu wazima kutorudishwa nyuma na maneno ya kukatisha tamaa yanayosemwa na  ya baadhi ya Wanajamii.

Amesema kuna baadhi ya Wanajamii wanaona kisomo cha Watu Wazima nikupoteza muda na kudhalilika jambo ambalo Mratibu huyo amesema sio sahihi badala yake ni ukombozi kwa waliokosa huduma hiyo katika umri wao wa utotoni.

Lee más…

ZIARA YA KUSHTUKIZA

Detalles
04 Septiembre 2023
323

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Bw. Khamis Abdulla Said, amefanya ziara ya Kushtukiza katika Skuli ya Sekondari Mwera, ili kuona changamoto zinazowakabili nakuzitafutia ufumbuzi. Katika ziara hiyo, pia Katibu Mkuu ameonana na Walimu wanofanya mafunzo kwa vitendo na kuwataka kuacha kufanya kazi kwa mazowea. Imetolewa na Kitengo cha Habari na Mawasiliano (WEMA).

Серед позичальників популярною послугою став мікрокредит онлайн на картку в мікрофінансовій організації. В банках такого поки що нема. Как в сегодняшних реалиях оформить микрозайм без отказа с мгновенным решением? Посмотрите лучшие предложения на нашем сайте.

ZIARA YA KATIBU MKUU KATIKA SKULI ZINAZOENDESHA HUDUMA ZA DAKHALIA

Detalles
01 Septiembre 2023
332

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar bwana Khamis Abdulla Said  Leo Tarehe 3108/2023 amefanya ziara katika Skuli zinazoendesha huduma za dakhalia kwa Mkoa wa Mjini Magharib.


Lengo la ziara hiyo ni kuangalia mazingira wanayoishi Wanafunzi hao ambao wanajiandaaa na mitihani yao ya Taifa.


Sambamba na hayo Bwana said alipat fursa ya kwenda kuona mazingira ya Skuli ya Sekondari Dkt salmin amaour ya chumbuni kutokana na kadhia iliojitokeza ya mwanafunzi uumia Bada ya kupandisha mashetana  na kujitupa.

Página 11 de 19

  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15

Contact Details

P.O.Box 394 Mazizini, Zanzibar
+255 24 223 2827
info@moez.go.tz

Main Menu

  • Home
  • About Us
  • News and Events
  • Staff Mail
  • Contact Us

Get in Touch

P.O.Box 394 Mazizini, Zanzibar
info@moez.go.tz

Our Institute

  • Kwarara Media Education Centre (KMEC)
  • The State University of Zanzibar (SUZA)
  • Vocational Training Authority(VTA)
  • Zanzibar Higher Education Loan Board(ZHELB)
  • Karume Institute of Science and Technology(KIST)
  • Zanzibar Examination Council(ZEC)
  • Zanzibar Institute of Education(ZIE)

External Links

  • Ministry of Education, Science and Technology (MOE)
  • The National Examination Council of Tanzania (NECTA)
  • The National Council for Technical Education (NACTE)
  • Tanzania Commission for University (TCU)
© MoEVT. Designed by ICT-Department.