• ZEAS
  • EMIS
  • E-OFFICE
  • AJESR
  • ZanVibali
MOEVT
  • Home
  • About Us
  • News and Events
  • Staff Mail
  • Contact Us
  1. You are here:  
  2. Home
  3. News and Events

MOEVT NEWS&EVENTS

Maonesho ya 4  yataleta Mafanikio Makubwa kwa Wanafunzi Kujua Fani zenye Soko la Ajira Duniani.

Details
02 August 2023
486

Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar Mhe.Simai  Mohamed Said amesema maonesho ya 4  yataleta mafanikio makubwa kwa Wanafunzi wengi kujua namna ya kujiunga na fani zenye soko la ajira duniani.

Amesema hayo wakati alipotembelea mabanda mbalimbali ya maonesho ya Nne ya wiki ya Elimu Zanzibar huko Maisara Mkoa wa Mjini Magharib Unguja.

Amesema uwepo wa taaluma ambayo itasaidia Wanafunzi kujua vipaombele vya Serikali ili taifa lizalishe wataalam wazalendo.

Read more …

Uhaba wa Wataalamu wa wa Sayansi nchini hupelekea kuzorotesha kasi ya Maendeleo.

Details
02 August 2023
419

Uhaba wa Wataalamu wa wa Sayansi nchini hupelekea kuzorotesha kasi ya Maendeleo.

Amesema hayo Daktari bingwa wa Meno Zanzibar. Dr  Semeni Shaabani Mohammed ambae ni Mtu wa Mfano alliyefanikiwa katika Masomo ya Sayansi (Role Model). wakati wa muendelezo wa  Ziara ya kuwahamasisha Wazazi katika kuwaandaa Watoto wa Kike kuyapenda na kuyasoma Zaidi Masomo ya Sayansi.


Ziara  hiyo imefanyika katika Skuli ya Mtoni Kigomeni, Mwenge, Mfenesi, Bubwini Makoba, Donge na Muwanda kwa Upande wa Unguja.

Amesema, Dunia  Sasa inaendana na Kasi ya Maendeleo ya Sayansi na Teknolojia hivyo Wanafunzi lazima wasome kwa bidii ili kupata wataalamu watakaoisaidia nchi kuendana na kasi ya maendeleo.

Read more …

Ziara ya Kutembelea miradi ya ujenzi inayoendelea katika Mkoa wa Kaskazini Unguja.

Details
02 August 2023
450

Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe Ali Abdulgulam Hussein amesema  atahakikisha anafuatilia miradi yote iliyopo chini ya Wizara ya Elimu ili ipatikane kwa wakati.

Ameyasema hayo wakati alipofanya ziara ya kutembelea miradi ya ujenzi inayoendelea katika Mkoa wa Kaskazini Unguja.

Amesema  ili miradi  ipatikane kwa wakati ni lazima kuwepo kwa mashirikiano baina ya Wizara na Wakandarasi waliopewa miradi hiyo sambamba na ufuatiliaji wa  mara kwa mara ili kuweza kuskiliza na kuzipatia ufumbuzi wa haraka changamoto mbalimbali zinazijitokeza katika miradi hiyo.

Read more …

Hafla ya Ugawaji wa Vifaa vya Maabara kwa Skuli ya Sekondari Jongowe, Tumbatu

Details
02 August 2023
400

Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe Ali Abdulgulam Hussein   amesema Serikali itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo ili kuhakikisha sekta ya Elimu inaendelea kupiga hàtua.

Amesema hayo wakati wa hafla ya Ugawaji wa vifaa vya maabara kwa Skuli ya Sekondari Jongowe Wilaya ndogo Tumbatu Mkoa wa Kaskazini Unguja.

Amesema  Serikali ya awamu ya nane imekusudia kuboresha miundombinu  ya Skuli na upatikanaji wa vifaa vya kufundishia ili taifa lizalishe wataalam wazalendo.

Aidha amesema upatikanaji wa vifaa vya kufundishia vitaleta ufanisi katika kukuza kiwango cha ufaulu nchini.

Read more …

UFUNGUZI WA MAONESHO YA NNE YA WIKI YA ELIMU YA JUU ZANZIBAR.

Details
02 August 2023
469

Spika wa Baraza la Wawakilishi, Mhe.  Zubeir Ali Maulid amesema,  jitihada zinazochukuliwa na Serikali katika kujenga hamasa kwa Wanafunzi kusoma na kupata matokeo yaliyokuwa bora.

Ameyasema hayo alipokuwa akifungua Maonesho ya Juma la Elimu ya Juu kwa niaba ya Makamo wa Pili wa Rais huko Maisara, amesema, Maonesho hayo ni sehemu ya ubunifu wa Wizara ya Elimu katika kukuza huduma za kielimu.

Amesema, Serikali imekuwa inahitaji Wataalamu wa sekta mbali mbali ili kuendelea kufanya kazi nchini.

Amesema, hatua ya Wizara ya Elimu kuweka Maonesho hayo itafikiwa lengo ikiwemo Wanafunzi kujifunza kupitia Maonesho hayo ikiwemo kujua namna bora ya kujiunga na Vyuo mbalimbali vilivyopo nchini.

Read more …

Page 14 of 18

  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18

Contact Details

P.O.Box 394 Mazizini, Zanzibar
+255 24 223 2827
info@moez.go.tz

Main Menu

  • Home
  • About Us
  • News and Events
  • Staff Mail
  • Contact Us

Get in Touch

P.O.Box 394 Mazizini, Zanzibar
info@moez.go.tz

Our Institute

  • Kwarara Media Education Centre (KMEC)
  • The State University of Zanzibar (SUZA)
  • Vocational Training Authority(VTA)
  • Zanzibar Higher Education Loan Board(ZHELB)
  • Karume Institute of Science and Technology(KIST)
  • Zanzibar Examination Council(ZEC)
  • Zanzibar Institute of Education(ZIE)

External Links

  • Ministry of Education, Science and Technology (MOE)
  • The National Examination Council of Tanzania (NECTA)
  • The National Council for Technical Education (NACTE)
  • Tanzania Commission for University (TCU)
© MoEVT. Designed by ICT-Department.