Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe Lela Muhammed Mussa amesema,  Wizara  Inathamini jitihada za Wadau mbali mbali katika Sekta ya Elimu ili kuleta maendeleo mazuri ya Elimu Zanzibar.

Ameyasema hayo wakati wa Ufunguzi wa Dahali ya Kisasa ya  Wanawake iliyo jengwa na Tasisi ya korea Food for the Hungry International  (KFHI ) chini ya Ufadhili wa Ushirika wa Maendeleo  Korea International Coperation Agency iliyoko huko Paje Mtule Wilaya ya Kusini Unguja.

Amesema, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Zanzibar imekuwa ikipokea misaada mbali mbali kutoka Kwa wadau mbali mbali ili kuweza kuboresha maendeleo ya Elimu Zanzibar.

Amesema, Wizara itaendelea  kutoa mashirikiano na Wadau wa Maendeleo katika Sekta ya Elimu ili kuweza kudumisha umoja na  mashirikiano katika    kuiboresha Sekta ya Elimu pamoja na sekta nyengine zote za kimaendeleo.

Aidha Waziri Lela, amesema Serikali ya Awamu ya nane chini ya Ungozi wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinfuzi Dkt Hussein Ali Mwinyi kipao mbele chake ni Elimu hivyo Wizara itahakikisha inatoa Elimu Bora  bora ili dhamira ya Serikali iweze kufikiwa  lengo.

Aidha, Waziri Lela  amewataka  Wanafunzi  kuitunza dahalia hiyo ili iweze kutumika kwa muda pamoja na  kuongeza jitihada ili wafaulu vizuri mitihani yao.

Aidha amewashukuru wafadhili hao kwa kuunga mkono Sekta ya Elimu Zanzibar na kuahidi  kuzithamini juhudi hizo ili kuleta mafanikio ya Elimu Nchini.

Mapema, Mkurugenzi Mtendaji wa KOICA nchini Tanzania Mr Mansik Shin amesema wamedhamiria kuboresha mazingira ya kujifunzia kwa watoto wa kike kwa. Lengo la kuwajea Mustakbali mzur wa maisha yao baadae.

Nae Mkurugenz Mtendaji wa Tasisi  ya Wanawake Initiative foundation (MIF )Bi Sabra Muhammed amesema Tasisi imekabidhi Magodoro 1881, Sukari Tani Tano na Robo, Unga , Mchele na Mafuta kwa skuli zote 35 zilizopo Mkoa wa Kusini Unguja kwa ajili ya kusaidia Wanafunzi wa Kidato cha Nne ambao ambao wapo Kambini. PVC täispuhutavad kummipaadid hea hinnaga siin

Amesema ni Mwaka Mmoja Tangu ianzishwe Tasisi ya Mwanamke Initiative Foundation lengo lake ni Kukuza Ufaulu na  kutokomeza Sifuri kwa Wanafunzi katika Mkoa wa kusini Unguja.

Amesema, katika kuhakikisha Ufaulu unaengezeka kwa Mkoa wa Kusini Unguja Tasisi hiyo inakusudia kufanya juhudi mbali mbali ikiwemo kuwapatia Mafunzo Maalum  Walimu wote na Wanafunzi pamoja na vifaa vitakavyo wasaidia pindi wanapo durusu masomo yao.