• EMIS
  • E-OFFICE
  • Home
  • About Us
  • News and Events
  • Staff Mail
  • Contact Us
  1. You are here:  
  2. Home
  3. News and Events

MOEVT NEWS&EVENTS

HAFLA YA UFUNGUZI WA MAFUNZO YA HATUA YA KWANZA YA KUWAANDAA WANAFUNZI WA AFYA

Details
12 September 2023
149

Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe Ali Abdulgulam Hussein  amesema kuwaandaa Wanafunzi kimasomo  kutapelekea kuzalisha wataalamu wenye ufanisi katika fani mbalimbali nchini.

Amesema hayo wakati wa hafla ya ufunguzi wa mafunzo  ya hatua ya kwanza ya kuwaandaa Wanafunzi wa  afya  huko  Zanzibar school of health ZSH Kwa Mchina Mwanzo  Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja.

Amesema kumuandaa  Mwanafunzi  mapema kimasomo ni kumjengea mustakabali mwema katika maisha yake ya Chuo Kwa kipindi chote Cha masomo.

Aidha Mhe Gulam amesema, Wizara ya Elimu kupitia Bodi ya Mikopo iko mbioni kurekebisha Sheria za mkopo ili na wanafunzi wa diploma na waweze kunufaika na mikopo hiyo. Amesema hatua hiyo itasaidia vijana wengi nao kuweza kutumia fursa za masomo.

Read more …

MAFUNZO MALUUM YA KUWAJENGEA UWEZO MAAFISA VIUNGO WA MRADI WA SEBEP

Details
12 September 2023
103

Serikali inaendelea kuimarisha miundombinu na kitekeleza Miradi ya kimkakati  ili kuiwezesha Zanzibar kutumia rasilimali zake ili kufikia malengo ya uchumi wa bluu.

Ameyasema hayo wakati akifungua Mafunzo Maluum ya kuwajengea uwezo maafisa viungo wa Mradi wa Sebep katika suala zima la ujumuishaji wa kijinsia katika ukumbi wa Mikutano Chuo Kikuu cha Taifa (SUZA) Kampasi ya Maruhubi Mkoa wa Mjini Maharibi 

Amesema mradi huo utasaidia Taifa kufikia malengo yake kutokana na mazingira ya nchi. Pia amesema mafanikio ya mradi huo yatafikiwa kwa wakati na ufanisi iwapo utazingatia masuala ya jinsia.

Read more …

UFUNGUZI WA MAFUNZO KWA WALIMU WAKUU NA WASHIKA FEDHA WA SKULI ZA SEKONDARI UNGUJA

Details
11 September 2023
118

Mkurugenzi Idara ya Elimu Sekondari Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar bi Asya Iddi Issa amesema kupewa Mafunzo ya kuisimamia na kutunza kumbukumbu ya matumuzi ya fedha kutawasaidi kutimiza majukumu yao.


Hayo ameyasema wakati wa kufungua Mafunzo kwa Walimu Wakuu na washika fedha wa Skuli za Sekondari Unguja Katika ukumbi wa mikutano Skuli ya Dk Ali Mohamed Shein Wilaya ya Mjini Unguja.


Amesema Mafunzo hayo kwa Walimu kutawasaidia  kuweza kupanga utaratibu mzur wa matumuzi ya fedha kwa kila mwaka.


Pia aliwasisitiza washika fedha hao kuhakikisha  wanatunza risiti za matumuzi katika Skuli zao kwani ndio njia itakayoonesha matumizi ya fedha za Serikali.

Read more …

HAFLA FUPI YA KUWAAGA WANAFUNZI WALIOPATA NAFASI ZA MASOMO NCHINI RAS EL KHEMA

Details
11 September 2023
100

Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe Ali Abdulgulam Hussein amesema Serikali ya Awamu ya Nane chini ya uongozi wa Mhe Dkt Hussein Ali Mwinyi inatumia kila jitihada kuekeza katika sekta ya Elimu ili kuzalisha vijana wenye katika fani  mbalimbali.


Amesema hayo wakati wa hafla fupi ya kuwaaga Wanafunzi waliopata nafasi za masomo nchini Ras el khema katika ukumbi wa mikutano Mazizini Unguja.


Amesema Serikali kupitia Wizara ya Elimu  inatumia fursa mbalimbali kwa kuhakikisha Wanafunzi wanasoma kwa kutumia mikopo na ufadhili mbalimbali ili taifa lizalishe wataalam wazalendo.


Amesema ni imani ya Wizara kwa Wanafunzi waliopata daraja la awali watapata ufadhili wa masomo hasa masomo ya sayansi kutokana na kuwepo kwa fursa mbalimbali.

Read more …

UTIAJI SAINI MKATABA WA UJENZI WA SKULI ZA GHOROFA NA KAMPUNI YA ROK DEVELOPMENT

Details
11 September 2023
62

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Bw. Khamis Abdulla Said,  ametiliana saini Mkataba wa Ujenzi wa Skuli za Ghorofa na kampuni ya  Rok Development kutoka nchini Uturuki,  katika Ukumbi wa Mikutano wa Wizara hiyo Mazizini Unguja.


Skuli hizo zitakazojengwa kwa kutumia Teknolojia ya Kisasa, zitajegwa katika maeneo mbalimbali ya Unguja na Pemba.


Katika hafla hiyo walihidhuria Watendaji Wakuu kutoka Taasisi ya Afisi ya Raisi Ufuatiliaji na Usimamizi wa Utendaji Serikalini (PDB) Dkt.Josephine Kimaro na Dkt. Ibrahim Kabole.


Imetolewa na Kitengo cha Habari na Mawasiliano(WEMA).
Tarehe:7/09/2023.

Page 2 of 12

  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10

Contact Details

P.O.Box 394 Mazizini, Zanzibar
+255 24 223 2827
info@moez.go.tz

Main Menu

  • Home
  • About Us
  • News and Events
  • Staff Mail
  • Contact Us

Get in Touch

P.O.Box 394 Mazizini, Zanzibar
info@moez.go.tz

Our Institute

  • Kwarara Media Education Centre (KMEC)
  • The State University of Zanzibar (SUZA)
  • Vocational Training Authority(VTA)
  • Zanzibar Higher Education Loan Board(ZHELB)
  • Karume Institute of Science and Technology(KIST)
  • Zanzibar Examination Council(ZEC)
  • Zanzibar Institute of Education(ZIE)

External Links

  • Ministry of Education, Science and Technology (MOE)
  • The National Examination Council of Tanzania (NECTA)
  • The National Council for Technical Education (NACTE)
  • Tanzania Commission for University (TCU)
© MoEVT. Designed by ICT-Department.